Bodi ya Maji, Bonde la Wami/Ruvu ni miongoni mwa Bodi za maji Tisa zilizopo nchini, Bodi hii ilianzishwa mwaka 2002, kufuatia sheria ya matumizi ya Maji (water utilization) Na. 42 ya mwaka 1998 na sheria hii ilifikia ukomo baada ya kuanzishwa kwa Sheria ya Usimamizi wa Rasilimali za maji Na.11 mwaka 2009 na marekebisho ya sheria No.8 ya 2022.
Kama yalivyo mabonde mengine Tanzania Bara, Bodi hii ilitangazwa kwenye gazeti la serikali No.2
Bodi inatekeleza majukumu yake katika mikoa sita ambayo ni Mororgoro, Dar es salaam, Pwani, Dodoma, Tanga na Manyara huku zote zikiwa na jumla ya Wilaya 27.
Jina la Wami/Ruvu lilitikana na mito 2 mikubwa inayopatikana katika eneo lake la utawala ambayo ni Mto Wami na Mto Ruvu.
Bonde lina eneo la 66,899 km2 ambayo iko katika mashariki ya kati ya nchi yenye idadi zaidi ya watu 12 Milioni. Bonde la Wami/Ruvu lina mabeseni matatu madogo ambayo ni Wami, Ruvu na Pwani. Kila moja ya mabeseni ya Wami na Ruvu yamegawanywa zaidi kihaidrolojia kama ifuatavyo Sehemu za maji ya kidakio cha Wami (44,233km2), Kinyasungwe (16,538km2), Mkondoa (12,960 km2), Wami (14,735 km2), Ruvu(17,843 km2) Ngerengere (km2,913 km2) huku kidakio cha Pwani (4,823km2)
Kwa hiyo, kila bonde linahitaji tathmini tofauti, tafiti na mipango kwa kuzingatia makadirio ya takwimu zilizotolewa na Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania (NBS).
Idadi ya wakazi wanaoishi katika Bonde la Wami/Ruvu ilikuwa takriban milioni 9.35 mwaka 2016. Hali ya hewa ya Bonde la Wami/Ruvu limebainishwa kuwa “maeneo mengine ya tropiki” kutokana na uhamiaji wa Eneo la Muunganiko wa Kitropiki (ITCZ). Wastani wa mvua kwa mwaka hutofautiana kutoka 1100 mm katika pwani hadi 600 mm ndani ya nchi. Kiwango cha juu cha mvua cha wastani cha kila mwaka hutokea katika Milima ya Uluguru na Nguru.
Eneo la pwani lina sifa ya misimu miwili ya mvua ilhali maeneo ya bara yana unimodal aina ya mvua.
Kuwa Bonde lenye mazingira safi na kijani linalotunza na kuendeleza vyanzo vya maji kwa maendeleo ya binadamu, kijamii na kiuchumi yanayostahimili majanga yanayotokana na maji.
Kuratibu kwa ufanisi mipango pamoja wa utunzaji na uendelezaji wa vyanzo vya maji ili kufikia maendeleo endelevu, jumuishi na stahimilivu ya Bonde.
"Tone la maji lazima lihifadhiwe."
Tunazingatia utamaduni wa Bodi unaothamini uasili wa uvumbuzi na ubunifu katika kukuza vipaji kwa kuzingatia uwazi na ari.
Tunafanya kazi kwa uwazi na taasisi za umma na wadau wengine huku tukibadilishana taarifa, maarifa, uzoefu na tukitambua kuwa tunategemeana kwa utunzaji wa vyanzo vya maji..
Tunazingatia ubora wa kazi kwa kiwango cha juu na kutoa huduma bora kwa wadau wetu.

