WIZARA YA MAJI NA WATERNET WAJADILI KUIMARISHA MIKAKATI YA UHIFADHI WA BWAWA LA MINDU.

Wizara ya Maji imefanya kikao cha pamoja na wawakilishi kutoka World Waternet, WRBWB pamoja na Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Morogoro (MORUWASA). Kikao hicho kimejikita katika kuimarisha ushirikiano kati ya taasisi hizo, hususan katika masuala ya uhifadhi wa mazingira kwenye vyanzo vya maji, ikiwemo Bwawa la Mindu ambalo ni chanzo kikuu cha maji kwa wakazi wa Mkoa wa Morogoro. Aidha, kikao kimeweka msisitizo katika kupan...







