emblem
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Wizara ya Maji
Bodi ya Maji Bonde la Wami/RUVU
ega Logo
Habari
ega-svg-tree

Bodi ya Maji Bonde la Wami/Ruvu kwa kushirikiana na Shirika la Kimataifa la Uhifadhi wa Mazingira (IUCN) imefanya kikao cha uelimishaji kwa wananchi wa mitaa ya Mundu na Kilala kuhusu zoezi la uwekaji wa Mipaka ya Makatazo kando ya Mto Mzinga. Lengo la kikao hicho ni kuwajengea wananchi uelewa kuhusu umuhimu wa uwekaji wa mipaka ya makatazo itakayowekwa pembezoni mwa Mto Mzinga, pamoja na kueleza namna zoezi hilo litakavyotekelezwa....

Soma Zaidi

Bodi ya Maji Bonde la Wami/Ruvu kupitia Kamati ya Maji ya Kidakio cha Wami, ikiongozwa na Mwenyekiti wake Hamza Sadiki, imefanya Kikao cha Pili cha Kamati hiyo kwa lengo la kufanya tathmini ya utekelezaji wa Mpango Kazi wa mwaka wa fedha 2025/2026 pamoja na kujadili na kupitisha Mpango Kazi wa mwaka wa fedha 2026/2027. Kikao hicho, kimewakutanisha wajumbe wa Kamati ya Maji ya Kidakio cha Wami ambapo wamepitia kwa kina taarifa ya utekelez...

Soma Zaidi

Bodi ya Maji Bonde la Wami/Ruvu imeanza rasmi utekelezaji wa shughuli zake kwa mwaka wa fedha 2026/2027 ikiwa na dhamira ya kuimarisha usimamizi endelevu wa rasilimali za maji na kuongeza utoaji wa huduma kwa wananchi katika maeneo yote ya Bonde la Wami/Ruvu. Katika mwaka huu wa fedha, Bodi itaendelea kutekeleza shughuli mbalimbali zinazolenga kulinda na kuhifadhi vyanzo vya maji, kutoa elimu kwa umma kuhusu matumizi sahihi na uhifadhi w...

Soma Zaidi

MOROGORO, Julai 2, 2026 Watumishi wa Bodi ya Maji Bonde la Wami/Ruvu wametakiwa kuanza mwaka wa fedha 2026/2027 kwa kuzingatia uwajibikaji, nidhamu ya kazi na matumizi sahihi ya mifumo ya utendaji ili kuongeza ufanisi katika utekelezaji wa majukumu ya taasisi. Maelekezo hayo yametolewa na Kaimu Mkurugenzi Bi. Janeth Kisoma katika kikao cha watumishi kilichofanyika katika Makao Makuu ya ofisi za Bodi ya Maji Bonde la Wami/Ruvu mkoani...

Soma Zaidi

  Kamati ya Kidakio cha Ruvu ikiongozwa na Mwenyekiti wake Bi. Praxeda Kalugendo imefanya kikao chake cha kawaida kwa lengo la kutathmini utekelezaji wa shughuli mbalimbali na kuweka mikakati ya kuboresha utendaji kwa mwaka wa fedha ujao. Katika kikao hicho wajumbe wamepitia taarifa ya utekelezaji wa kazi kwa mwaka wa fedha 2025/2026 ambapo wamejadili mafanikio yaliyopatikana pamoja na changamoto zilizojitokeza katika kipindi...

Soma Zaidi
Mpangilio

slot gacor