WAMI/RUVU WATOA ELIMU KUHUSU UWEKAJI WA MIPAKA YA MAKATAZO.

Bodi ya Maji Bonde la Wami/Ruvu kwa kushirikiana na Shirika la Kimataifa la Uhifadhi wa Mazingira (IUCN) imefanya kikao cha uelimishaji kwa wananchi wa mitaa ya Mundu na Kilala kuhusu zoezi la uwekaji wa Mipaka ya Makatazo kando ya Mto Mzinga. Lengo la kikao hicho ni kuwajengea wananchi uelewa kuhusu umuhimu wa uwekaji wa mipaka ya makatazo itakayowekwa pembezoni mwa Mto Mzinga, pamoja na kueleza namna zoezi hilo litakavyotekelezwa....







